SUMAYE;CCM NJIA PANDA UCHAGUZI 2015 HABARI KAMILI HII HAPA by nasanyo fortnine

Rushwa kuiweka CCM njiapanda
CHAMA
Cha Mapinduzi (CCM) kipo hatarini kukumbwa na mpasuko mkubwa pindi
chama hicho kitakapomsimamisha mgombea urais katika Uchaguzi Mkuu wa
mwaka 2015 ambaye anapenda vitendo vya rushwa.
Hali hiyo
inadhihirishwa na Waziri Mkuu Mstaafu wa awamu ya tatu, Frederick
Sumaye, ambaye ameweka wazi kwamba atakihama chama hicho endapo kwenye
Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 atasimamishwa mgombea anayependa vitendo vya
rushwa.
Sumaye aliyasema hayo
jana wakati akihojiwa katika kipindi cha Medani za Siasa na Uchumi,
kilichorushwa hewani na Kituo cha Televisheni cha Star TV.
Alisisitiza kuwa mtu
anayetoa rushwa hawezi kuwatumikia wananchi, hivyo yeye atahama CCM
endapo kwenye Uchaguzi wa Mkuu wa mwaka 2015 atasimamishwa mgombea
anayependa vitendo vya rushwa.
Alisema, siasa za
Tanzania kwa sasa zimekuwa fedha kwani kama mtu huna fedha huwezi
kuchaguliwa; jambo ambalo ni hatari kwa maendeleo ya nchi na
tusipoangalia basi nchi itapata anguko kubwa.
Sumaye alisema kama
utaratibu huo utaendelea wa kwamba mwenye fedha ndiye anaongoza nchi,
basi Watanzania wajiandae kuumia, kwani mtu huyo anakuwa hana machungu
na nchi yake, mwishowe ataongoza nchi kwa kutumia rimoti, ambapo ikiwa
amepewa sh. milioni 10 za kufanyia kampeni na akawa kiongozi sasa huyo
mtu atawezaje kumshurutisha alipe kodi? Matokeo yake ni wenye fedha ndio
wataendesha Serikali.
Alisema endapo mtu ana
vigezo vya kuwa kiongozi, basi haina haja ya kutoa ruswa, kwani wananchi
wenyewe ndio wanaona utendaji wake."Hata wananchi wanajua kuwa mtu
akiingia madarakani kwa kutoa rushwa anakuwa hana moyo wa kuwatumikia,
bali anajali masilahi yake binafsi," alisema Sumaye na kuongeza;
"Siwezi kuwakataza
wananchi kuchukua fedha watakazopewa na wagombea wachukue, lakini
wasiwachague,tukifanya hivyo vitendo vya rushwa vitapungua."
Alisema, Serikali
nyingi duniani zimeanguka kwa mfumo huo na kwamba kama hali hiyo
itaendelea nchini, CCM itakufa. Aliongeza kwamba;
"Mtu kama unajiona wewe
ni mrefu kwa nini uongeze tofali,mtu huyo anaweka tofali ili aweze
kuvifikia virefu wakati hana sifa za kufika atakapo, hata hawa viongozi
watoa rushwa ndio walivyo hawana vigezo lakini wanataka kulazimisha
wafike wanapotaka."
Alifafanua kwamba;
"Jamii ina hasira,jiulize kwa nini watu hawachomi boda boda na wakati
huo wanaenda kuchoma gari la mbunge, ni kwamba watu wamechoka na
matabaka yanayowekwa na viongozi."
Alisema njia mojawapo
ya kukomesha rushwa ni kutomchagua anayetoa hongo na kuonya kwamba kama
vitendo hivi vitaendelea basi hata CCM kitapata pigo na nchi yenyewe
itaenda mrama.
Aliongeza kuwa, uchumi
wa Tanzania uko kwenye mikono ya watu wachache, jambo ambalo ni hatari
kwa maendeleo ya nchi na kumtaka Rais anayekuja aangalie jinsi ya
kulitatua hilo tatizo.
"Anayetakiwa kulipa kodi, basi alipe kodi ili pawepo na usawa kati ya wenye nacho na wasio kuwa nacho," alisema Sumaye.
.Akiongelea suala la
mgombea urais kwa mwaka 2015, alisema ujana na uzee si sifa ya mtu kuwa
rais bali kinachotakiwa ni mtu kuwa na vigezo vya kuweza kuongoza Taifa.
"Kama tunamwona an a
nguvu,maadili, mchapakazi na anatetea masilahi ya Taifa, basi tumchague
lakini si kigezo cha wewe ni mzee au kijana ndio tukupe nafasi wakati
huna vigezo,"alisema Sumaye.
Alisema suala la Rais
kutakiwa kuwa kijana au mzee lisiwapotezee muda watu, kwani suala hilo
linataka kuwaondoa kwenye ajenda ya msingi ya kupata Rais anayefaa.
"Sifa za urais zipo na
ili mtu agombee lazima jamii ikuone unafaa na una kila kigezo kwa hiyo
mambo ya sijui rais awe kijana au mzee lisitupotezee muda, kwani
litatuondoa kwenye hoja ya msingi,"alisema Sumaye.
Alisema katika utawala
wa awamu ya tatu Serikali ilibana sana matumizi ya Serikali, hali
iliyosaidia nchi kuwa na fedha za kutosha na kusababisha kudai kuwa Rais
Mstaafu Benjamin Mkapa, ameficha fedha nje ya nchi.
"Mimi nilichapa kazi
kweli kweli kwa kuwa ndio nilikuwa msimamizi mkuu na tangu niteuliwe
nafasi ya Waziri Mkuu kwa miaka 10 sikuwahi kwenda likizo, hivyo muda
ukifika nitagombea au sitagombea na nikiwa rais au nisiwe rais
nitaendeleza mapambano dhidi ya rushwa," alisema Sumaye.
0 comments: