MUFTI WA MISRI SHAWKY ALLAM ALAANI WATU WANAOBOMOA MAKABURI YA MITUME HUKO IRAQ by nasanyo fortnine
Mufti wa Misri Shawky Allam amelaani vitendo vya wanachama wa
kundi la kitakfiri la Daesh kushambulia na kubomoa maeneo matukufu
walipozikwa Mitume na Maimamu watukufu nchini Iraq, na kwamba vitendo
hivyo vinakinzana na mafundisho sahihi ya dini Tukufu ya Kiislamu. Allam
amesema kuwa, ni haramu kuwavunjia heshima Mitume na Maimamu watukufu
na waja wema kwa kubomoa makaburi yao. Mufti wa Misri ameitaka jamii ya
kimataifa kuingilia kati na kuzuia jinai hizo za kuwavunjia heshima watu
waliokwishatangulia mbele ya Haki. Amesisitiza kuwa, wanamgambo wa
kundi la Daesh wameshindwa kabisa kufahamu mafundisho sahihi ya Uislamu
sambamba na kushindwa kusoma historia ya Mtume wa Uislamu Muhammad
(SAW). Kwengineko jeshi la Iraq limetangaza kuwa, limeinua bendera
katika jingo la ikulu ndogo ya rais katikati mwa mji wa Tikrit nchini
humo. Hayo yamethibitishwa na Wizara ya Ulinzi ya Iraq na kuongeza kuwa,
mafanikio hayo yamekuja baada ya makundi ya kigaidi kukimbia kufuatia
kushindwa na jeshi hilo kwa kushirikiana na vikosi maalumu vya kupambana
na ugaidi nchini humo. Kwa mujibu wa wizara hiyo, mapema leo asubuhi
jeshi la Iraq serikali na wapiganaji wa kujitolea walianzisha
mashambulizi makali ya anga na nchi kavu kwa lengo la kuukomboa mji huo
wa Tikrit dhidi ya wapiganaji wa Daesh na kufanikiwa kuyakomboa maeneo
mengi ya mji huo sambamba na kuzidhibiti ofisi za serikali na hospitali
ya mji huo, huku magaidi wa kitakfiri wa Daesh wakiishia kukimbia na
kuelekea maeneo mengine. Wizara ya Ulinzi ya Iraq imesisitiza kuwa hadi
sasa operesheni za kuusafisha kikamilifu mji huo na kuwasaka wanachama
wa kundi hilo la kigaidi, zingali zinaendelea.
USISAHAU KU LIKE PAGE YETU YA FACEBOOK
0 comments: