MJI WATEKWA NA WAASI HABARI KAMILI HII HAPA by nasanyo fortnine
by nasanyo fortnine

Wanajeshi wa serikali ya Sudan kusini wapiga doria.
Waasi nchini Sudan kusini wanasema kuwa wameuteka mji muhimu wa Nasir katika jimbo la upper Nile.
Wanasema kuwa wameuteka mji huo baada ya kushambuliwa na vikosi vya serikali.
Jeshi la Sudan Kusini limesema kuwa vita vinaendelea katika mji huo,ambao waasi wamekuwa wakishambulia tangu siku ya jumamosi.
Msemaji wa jeshi amesema kuwa huenda huo ukawa mwisho wa makubaliano ya kusitisha vita yaliotiwa sahihi mnamo mwezi May.
Mji wa Nasir ulikuwa makao makuu ya mda ya ya
kiongozi wa waasi Riek Machar ,ambaye alihudumu kama makamu wa rais wa
Sudan kusini kabla ya kutofautiana na rais Salva Kiir.
0 comments: