MELI YAZAMA NA WATU ZAIDI YA MIANNE (400) HUKO KOREA KUSINI habari kamili by nasanyo fortnine

Meli ya Korea Kusini iliyokuwa imewabeba zaidi ya abiria mianne ilizama kusini mwa pwani ya nchi
 hiyo Jumatano asubuhi 
 
Walioshuhudia ajali walisema kuwa walisikia kishindo kikubwa wakati meli hiyo ilipoanza kuzama
 
Wengi wa watu waliokuwa katika meli hiyo walikuwa wanafunzi waliokuwa katika ziara ya kisiwa kimoja
nchini humo
 
Watu wawili wameripotiwa kufariki ingawa shughuli ya uokozi ingali inaendelea. Wengine zaidi ya miatatu
 bado hawajulikani waliko
 
Wazazi, jamaa na marafiki wa wanafunzi waliokuwa katyika meli hiyo wanatizama kupitia televisheni picha
 za meli hiyo ilipozama
 
Wanafunzi wengi waliokolewa kupitia mashimo yaliyo kando ya meli hiyo huku wengine wakiruka baharini
 katika jitihada za kuokoa maisha yao
 
Inaarifiwa zaidi ya watu miatatu hawajapatikana , wengine 164 waliweza kuokolewa na watu wawili
 wamethibitishwa kufariki

0 comments:

Copyright © 2014 NASANYO BLOG