WAZIRI MSAAFU AKATA RUFAA YA ADHABU ALIYOPEWA habari kamili hii hapa by tuntu baby

  • Dodoma. Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye amekata rufaa
  •  Kamati Kuu ya CCM kupinga adhabu ya onyo kali aliyopewa na
  •  chama kutokana na madai ya kuanza kampeni za urais mapema
  •  kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu ujao.
  • Akizungumza na gazeti hili mjini Dodoma jana, Sumaye alisema
  •  kwa ufupi hakuridhishwa na adhabu hiyo na kuthibitisha hilo, tayari
  •  amekata rufaa.
  • Hata hivyo, alisema hadi jana hakuwa amepata mrejesho wowote
  •  kwa sababu kanuni hazielezi ni muda gani anatakiwa kuwa amepewa 
  • taarifa kuhusu rufaa hiyo.
  • Sumaye na wanachama wenzake, Edward Lowassa, Bernard Membe,
  •  Stephen Wassira, William Ngeleja na January Makamba walitiwa hatiani
  •  kwa kuanza kampeni mapema, hivyo kupewa onyo linalokwenda sambamba
  •  na kutowania nafasi yoyote ndani ya chama kwa miezi 12.
  • “Siwezi kuwazungumzia wenzangu, nazungumza kwa upande wangu, sikuridhishwa
  •  na adhabu hii na nimeshakata rufaa ingawa sijapata majibu yoyote, naendelea kusubiri
  • ,” alieleza Sumaye.
  • Waziri Sumaye alikataa kuzungumzia hali ya utekelezaji wa adhabu hiyo, akisema 
  • anachosubiri ni mwitiko wa rufaa yake aliyoiwasilisha Kamati Kuu ya CCM,
  •  mwanzoni mwa mwezi huu. “Sina kumbukumbu nzuri ilikuwa tarehe ngapi,
  •  lakini ni mwezi huu wa tatu.”
  • Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alipoulizwa juu ya 
  • rufaa hiyo alisema hana taarifa zaidi ya habari hizo kuzisikia kutoka kwa mwandishi.
  • Hata alipotakiwa kueleza nani anatakiwa kuwa na taarifa hizo, alisema: “Mimi ndiye
  •  msemaji wa chama, hakuna wa kuzungumzia suala hili zaidi yangu. Kwanza inatakiwa
  •  ijulikane, rufaa hiyo imepelekwa ngazi gani ya uongozi kwa sababu kila ngazi ina muda
  •  tofauti wa kufanya vikao vyake vya uamuzi.”
  • Nnauye baada ya kuelezwa kuwa rufaa ya Sumaye imewasilishwa Kamati Kuu ya CCM
  • , alisisitiza kuwa hana taarifa nayo na kwamba haiwezekani rufaa ipelekwe kwenye kikao
  •  kilichotoa adhabu husika.
  • Hata hivyo, Sumaye alisisitiza kuwa rufaa yake ameiwasilisha Kamati Kuu kwa mujibu wa
  •  kanuni zinazohusika.

0 comments:

Copyright © 2014 NASANYO BLOG