MGOMO MGOMO HII NI HABARI KAMILI MGOMO WA DALADALA MOROGORO by tuntu baby

 
MADEREVA wa daladala Manispaa ya Morogoro wamegoma asubuhi hii wakidai 
kukamatwa hovyo na matrafiki na hakuna daladala linalofanya safari yoyote katika
 manispaa hiyo.
Madereva hao wanadai wameamua kugoma kutokana na kamatakamata ya askari wa
 usalama barabarani, ambapo wamesema daladala moja kwa siku linaweza kukamatwa
 hadi mara nne na wakihoji wanaambiwa ni makosa tofauti.
Waliongeza kuwa wamepeleka malalamiko yao ngazi mbalimbali za serikali mkoani 
Morogoro bila mafanikio.
Mgomo huo umewaathiri zaidi wanafunzi ambao wapo katika mitihani ya nusu muhula
 ambapo baadhi yao walilazimika kutembea kwa miguu huku wengine wakirudi nyumbani kujipanga.
Ili kuongeza uzito katika mgomo huo, madereva hao wametoa tahadhari kwa wamiliki
 wa mabasi ya Abood kutojaribu kupeleka mabasi yao barabarani kama ambavyo
 wamekuwa wakifanya pindi ukitokea mgomo ndani ya manispaa hiyo.......
http://api.ning.com/files/UbQGb2BFO*VuOF18pjA2C*7MGWdBfxzjNNHFh4J*7dGTNWXacY1zgI20WPWZLbTdoj*I1ot5ZBqtKU4vqhyGhna2o6bDodR5/BREAKINGNEWS.gif



0 comments:

Copyright © 2014 NASANYO BLOG