YULE ALIYEMUUA MTOTO NA KUMLA UBONGO NAE AMEFARIKI HABARI KAMILI HII HAPA by nasanyo fortnine

Wananchi wakishuhudia mtuhumiwa wa mauaji Laurency Mramba akipandishwa kwenye gari kupelekwa Hospitali ya Kilema kwa ajili ya matibabu baada ya kujikata nyeti zake na kuzila
 
Moshi. Yanawezekana yakawa ni moja ya mauaji ya kutisha nchini, baada ya kijana mmoja kumuua mwanafunzi wa darasa la tatu Shule ya Msingi ya Marangu Hills Academy kisha kula ubongo wake.
Mbali na kula ubongo wa mtoto huyo, Francis Urassa (9), mtuhumiwa huyo Lawrence Mramba alijikata sehemu za siri kwa kutumia wembe na kuzila mithili ya mshikaki akikata kipande kimoja baada ya kingine.
Hata hivyo, mtuhumiwa huyo naye alifariki dunia saa chache baadaye baada ya kufikishwa Hospitali ya Kilema iliyopo Moshi Vijijini wakati madaktari na wauguzi wakimpatia matibabu.
Mashuhuda wa tukio hilo lililotokea jana saa 1:00 asubuhi Kijiji cha Samanga, Wilaya ya Moshi Vijijini, walidai kijana huyo alikuwa na nguvu za ajabu lakini baadae polisi walifanikiwa kumdhibiti.
Wananchi walipiga simu polisi kuomba msaada baada ya kijana huyo aliyekuwa na panga kuwazidi nguvu na kubakia watazamaji wakimwangalia namna anavyokula nyama za mwili wake.
Lilikuwa ni tukio lililovuta hisia za wakazi wengi waliokusanyika kijijini hapo huku wengine wakirekodi tukio la kijana huyo kula uume wake kwa kutumia simu za mikononi.
Polisi kutoka Mji wa Himo walifika eneo la tukio na kumkamata kijana huyo wakati huo akiwa katika hali mbaya kutokana na kupigwa kwa mawe na wananchi na kujikata sehemu mbalimbali.
Mwili wa kijana huyo ulionekana ukiwa umetapakaa damu kuanzia mdomoni hadi sehemu za siri kutokana na damu nyingi kuchuruzika wakati akijikata uume vipande vipande na kuula.
RPC Kilimanjaro anena
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz aliliambia gazeti hili jana kuwa chanzo cha tukio hilo ni upungufu wa akili uliomkumba kijana huyo na kuanza kuvunja vioo vya nyumba.
“Leo (jana) asubuhi alimkata huyo mtoto wa tajiri yake kwa panga na kisha na yeye akaanza kujikata sehemu zake za siri na kula baadaye akajikata pia sehemu mbalimbali za mwili,” alisema.
Kwa mujibu wa Kamanda Boaz, mtuhumiwa huyo alifariki katika Hospitali ya Kilema iliyopo Wilaya ya Moshi Vijijini wakati madaktari na wauguzi wa hospitali hiyo wakimpatia matibabu.
 

0 comments:

Copyright © 2014 NASANYO BLOG