MATESO ANAYOYAPATA MTOTO HUYU NI HATARI ANAOMBA MSAADA by nasanyo fortnine

UKISEMA wewe unateseka inawezekana hujawaona wanaoteseka. Kijana Peter Andrea (23)  mkazi wa Mlandizi, Bagamoyo, Pwani anaishi kwa mateso ya tumbo kuvimba kwa miaka 13 sasa huku akishindwa kusoma na kutekeleza ndoto za maisha yake ya baadaye.
 
Kijana Peter Andrea akiwa na uvimbe tumboni kwa miaka 13
Akizungumza kwa uchungu na Amani kuhusu mateso anayoyapata kwa kipindi 
chote
 hicho, Peter alisema matatizo hayo  yalianza kumkumba akiwa na miaka 10
 tangu kuzaliwa.
Alisema hali hiyo ilianza kwa kila siku akiamka kujikuta amevimba mwili, 
siku nyingine amevimba uso mpaka akafika hatua tumbo likashika nafasi 
ya moja kwa moja. “Nilikuwa nikiamka asubuhi najikuta nimevimba mwili, 
mara uso. Ikafika wakati tumbo nalo likavimba. Nimezunguka kwa madaktari 
tofauti na mama kipindi akiwa hai kwa bahati nzuri nikapona. Lakini nilikaa 
kidogo tu hali ikajirudia kama unavyoniona,”

 
Kijana 
Peter Andrea 
akiwa na Baba yake mzazi.
alisema Peter na kuongeza: “Baada ya mama  kufariki dunia nikawa 
naishi maisha ya kuzunguka na kuomba msaada kwa watu bila mafanikio.
 Mwaka 2013 nilipata msaada kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kibaha,
 akanipeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili (Dar) ambapo nilifanyiwa vipimo

na kugundulika nina matatizo kwenye ini, nikapewa dawa na kuhudhuria kliniki
“Baada ya vipimo vya mwanzo nilirudia tena kwa mara nyingine, niligundulika pia
 nina matatizo ya figo, moyo na kibofu cha

 
mkojo. Niliumia sana, niliia sana. Niliambiwa nikatumie dawa za mitishamba 
halafu niwe nakwenda kupima lakini nimetumia dawa.
hizo mpaka sasa sioni dalili yoyote ya kupona.”
Akaendelea: “Ninawaomba Watanzania wenzangu wajitokeze kunisaidia nipone 
kwani sijabahatika kusoma tangu nikiwa mdogo,

nimejitahidi kusoma elimu ya watu wazima (Memkwa) nimeishia darasa la pili, 
nawaomba mnisaidie jamani nateseka sana na haya

magonjwa karibu manne.”
ANAHITAJI MSAADA
Kama umeguswa na mateso ya Peter na unahitaji kumsaidia, wasiliana naye kwa 
simu namba 0716 782 682 au 0659 690 968

0 comments:

Copyright © 2014 NASANYO BLOG