HII NI MAANA HALISI YA PASAKA SOMA UPATE KUFAHAMU by nasanyo fortnine


Maana ya Pasaka kwetu leo. by nasanyo fortnine

Kwetu  leo Pasaka  inamaanisha mambo mawili.    Inamaanisha kwamba kuna njia ambayo
leo  tunaweza  kupata wokovu.   Wanadamu wote  ni waovu.    Tumezaliwa  tukiwa wenye
dhambi na tumeishi maisha ya dhambi.   Lakini hii haimaanisha kwamba ni lazima  tukufe
katika  dhambi  zetu.    Mungu  ametufungulia  njia  ambayo  tunaweza  kupata  wokovu. 
Unaweza kuwa mtu mwovu sana ambaye ameishi maisha yake yote akitumikia dhambi na
uwe  hujawahi  kuenda  kanisani  siku hata moja  au  kufanya  jambo  lolote  zuri.   Lakini hii
haimaanishi  kwamba  hakuna  tumaini  lolote.   Ujumbe wa  pasaka ni  ujumbe wa  tumaini. 
Huu ni ujumbe ambao unatueleza kwamba Mungu amefungua njia kwa watenda dhambi
kuja  kwake  ili  waweze  kuokoka.    Huhitaji  kubaki  katika  dhambi  zako,  unaweza
kuokolewa.
Pili, Pasaka inamaanisha kwamba wale wote ambao watakuja kwa Kristo Yesu kwa kutubu
na kwa  imani, wamehakikishiwa wokovu.    Ikiwa utakuja kwa Kristo Yesu  leo na uamue
kuacha dhambi zako, ukweli ni kwamba umehakikishiwa msamaha wa dhambi zako nafasi
mbinguni.  Ikiwa jutakuja kwake leo na umwombe msamaha wa dhambi zako na maisha ya
milele mbinguni, atakusikia na atakujibu.   Huu ndiyo ujumbe wa pasaka.   Ni ujumbe wa
tumaini la milele; ni ujumbe kwamba Kristo amaehakikisha wokovu wetu na maisha yetu
ya milele.
 Hii ndiyo maana halisi ya Pasaka; ni kifo na kufufuka kwa Kristo na ujumbe wa  tumaini
kwa wote ambao wanatafuta wokovu.

 “Kwa maana yale niliyopokea ndiyo niliyowapa ninyi, kama yenye
umuhimu wa kwanza: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu,
kama yasemavyo maandiko, ya kuwa alizikwa na alifufuka siku tatu” (1
Wakorintho 15:3-4).

Katika kifungu hiki cha Bibloia mtume Paulo anatueleza kuhusu ujumbe mkuu wa Biblia.
Anatuonyesha  kwamba  katika Biblia  kuna mambo  ambayo  ni  yanafaa  kupewa  umuhimu
zaidi.    Tunasoma  kuhusu mambo  haya  bi  gani.   Kwa  hivyo  Biblia  hatufunzi  tu  kuhusu
ujumbe muhimu wa Biblia,  bali  pia  inatufunza pasaka ni nini.   Kifungu hiki  kinatueleza
kwa nini ujumbe wa Biblia ni wa muhimu  sana na ni kwa nini  tunafaa kuuelewa vyema
sana na kuupokea kwa mioyo yetu yote.

1. Pasaka inahusu kifo cha Bwana Yesu Kristo.

Biblia  inasema  katika  kifungu  hiki  kwamba,  “Kwa  maana  yale  niliyopokea  ndiyo
niliyowapa ninyi, kama yenye umuhimu wa kwanza: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya
dhambi zetu, kama yasemavyo maandiko.”  Hii inamaanisha kwamba kifo cha Kristo Yesu
ndiyo tokeo la muhimu sana katika historia ya ulimwengu wote.  Wakati tunasoma Biblia
lazima tufahamu kwamba msingi wake wote ni kifo cha Yesu Kristo.

2. Pasaka inahusu kufufuka kwa Bwana Yesu Kristo.

Biblia  inasema  katika  kifungu  hiki  kwamba,  “Kwa  maana  yale  niliyopokea  ndiyo
niliyowapa ninyi, kama yenye umuhimu wa kwanza: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya
dhambi  zetu,  kama  isemavyo maandiko,  ya  kuwa  alizikwa  na  alifufuka  siku  ya  tatu”  (1
Wakorintho 15:3-4).

Lazima tukumbuke kwamba Agano la Kale lote linatuongoza kwamba Kristo Yesu na kifo
chake.    Tukumbuke  kwamba  waandishi  wa Mathayo, Marko,  Luka  na  Yohana,  wakati
waliandika  vitabu  hivi,  waliandika  wakituongoza  kwa  hili  tokea  moja,  yaani  kifo  cha
Bwana Yesu Kristo.  Kila sura ya vitabu hivi vine vya injili, inatuongoza kwa msalaba wa
kristo Yesu.  Nyaraka za mitume wote msingi wake ni kifo cha Kristo Yesu.  Ni kifo cha
Kristo Yesu ambacho kiliwaongoza kuandika ujumbe ambao waliandika.  Kifo cha Kristo
Yesu ndiyo tokeo la maana kabisa.

Katika  kifungu  hiki  tunaelezwa  kwamba  kifo  cha  Kristo  kiilikuwa  kimetabiriwa  katika
maandiko.   Hii  inamaanisha  kwamba Agano  la Kale  lote  linazungumzia  kifo  cha Kristo
Yesu kama tokeo kuu katika historia ya ulimwengu wote.  Hili ni tokeo ambalo lilitabiriwa
kwa  njia  tofauti  tofauti  katika  karne  zote.   Hili  ndilo  tokea  ambalo Mungu alizungumza
kuhusu  wakati  alimwambia  Shetani  kwamba,  “Atakuponda  kichwa,  nawe  utamgonga
kisigino”  (Mwanzo  3:15).    Hili  ndilo  tokea  ambalo  Mungu  alikuwa  anakudia  wakati
aliwamuru  Waisraeli  watoke  dhabihu  za  wanyama  katika  hekalu.    Sheria  ya  Musa
ilitayarisha njia ya kuja kwa kristo Yesu na kifo chake.

Sababu kwa nini kifo cha Kristo Yesu ni cha maana sana ni, kwa sababu kupitia kwa kifo
chake,  wanadamu  waokolewa  kutoka  kwa  dhambi  zao.    Biblia  inasema,  “Kristo  Yesu
alikuja ulimwenguni kuokoa wenye dhambi” (1 Timothy 1:15).  Hili ndilo likuwa kusdi la
Kristo kuja hapa ulimwenguni: kuwaokoa wenye dhambi kutokana na hatia na uchafu wa
dhambi.    Kifo  chake  na  kufufuka  kwake  ndiyo  njia  ambayo  inatuletea  wokovu  na
kutuingiza mbinguni.   Bila kifo na kufufuka kwa Kristo Yesu, hakuna wokovu kwa mtu
yeyote.    Hii  ndiyo  njia  ambayo Mungu  ameweka  ili  sisi  tupate  kuokoka  na  ndiyo  njia
ambayo tunafaa kutumiikiwa tunataka kuokoka.
 Ikiwa  hujaokoka,  utabaki  katika  dhambi  zako  hadi  utakapokuja  kwa  Kristo  Yesu  kwa
kumwamini.  Utabaki ukiwa hujaokoka hadi utakapoamini katika kifo na kufufuka kwake. 
Lazima umwombe Mungu akusamehe dhambi zako zote kupitia kwa kifo cha Kristo Yesu
msalabani kalvari.   Hii ndiyo njia ya pekee ya kupokea msamaha wa dhambi zako, yaani
kupitia kwa kifo cha Kristo Yesu msalabani.

Kama  tu  vile  kifo  cha Kristo Yesu  ndiyo msingi wa  ujumbe wa  injili,  vivyo  hivyo  pia
ndivyo  ilivyo  hata  kufufuka  kwake.    Paulo  aliwafundisha Wakorintho  kuhusu  kifo  na
kufufuka  kwa  Kristo  Yesu  kwa  sababu  alijua  kwamba  mambo  haya  ndiyo  msingi  wa
ujumbe wa injili.

Kufufuka  kwa  Bwana Yesu Kristo  kunamaanisha  kwamba Mungu  alikubali  dhabihu  ya
Kristo kwa ajili ya watenda dhambi.  Msalabani Kalvari Kristo alijitoa kwa ajili ya watenda
dhambi na damu yake  ili  iweze kuwaosha wenye dhambi kutoka kwa dhambi zao.   Hivi
ndivyo  Bwana Yesu kristo alikuwa anafanya msalabani.  Alikuwa anafanya kile ambacho
makuhani  wa  Agano  la  Kale  walikuwa  wanafanya  wakati  waliwatoa  wanyama  kama
dhabihu  kwa  ajili  ya  watu wote.   Walitoa wanayama  ambao  walikuwa  hai  ili watu wa
Isreali wasihukumiwe na Mungu.  Pia walitoa damu ili watu waweze kuoshwa kutoka kwa
dhambi zao.

Hivi ndivyo Bwana Yesu Kristo alifanya msalabani Kalvari kwa ajili ya watenda dhambi. 
Alitoa maisha  yake  kwa  ajili  ya  dhambi  zao  na  damu  yake  ili waweze  kuoshwa  dhambi
zao.   Kwa hivyo,  tunajua kwamba Mungu Baba alikubali dhabihu ya Kristo kwa  sababu
alimfufua  kutoka  kwa  wafu.    Kwa  kumfufua  kutoka  kwa  wafu,  Mungu  Baba  alikuwa
anasema  kwamba  yeyote  ambaye  atamwamini  Kristo  kwa  ajili  ya  wokovu  wake,
ataokolewa  kutoka  katika  dhambi  zake  na  kuhakikishiwa nafasi mbinguni.   Kwa  sababu
Kristo Yesu  alifufuka,  ako  na  uwezo  wa  kuwaokoa wote  ambao wanakuja  kwa Mungu
kupitia Yeye (Waebrania 7:25).
Kwa  sababu  Kristo  Yesu  alifufuka,  ni  dhihirisho  kwamba  Yeye  pekee  ndiye  njia  ya
wokovu kwa watenda dhambi.   Wakati Mungu Baba alimfufua Kristo kutoka kwa wafu,
alikuwa  anasema  kwamba, ni wale  tu  ambao wanakuja  kwake  kupitia  kwa Kristo  ndiyo
wataokoka.   Kwa  sababu  ni Yeye  ambaye Mungu  amempa mamlaka  ya  kuokoa.   Kuna
watu  wakuu  ambao  huwapataia  watu  Fulani  mamlaka  na  husema  kwamba  ikiwa  mtu
yeyote  anataka  kuwaona,  lazima mtu  apitie  kwa mtu  au watu  hao.    Ikiwa mtu  hatapitia
katika mtu huyu, basi hataweza kumwona mkuu huyo.  Kristo ndiye amewekwa na Mungu
kuwa Mwokozi wa  ulimwengu.    Tunajua  hili  kwa  sababu Kristo  ndiye  amefufuliwa  na
Mungu.   Kufufuka kwa Kristo Yesu  si kama  kule kwa Lazaro.   Lazaro hakupewa mwili
mpya ambao haungekufa  tena.   Baada ya miaka michache baada ya Lazaro kuregeshewa
uhai, alikufa tena.  Lazaro hauko hai leo katika mwili mpya.

ASANTE KAMA UNA MAONI USHURI TUMA TEXT KWA NAMBA HII +255 767 361 980 AU COMMENT HAPO CHINI

0 comments:

Copyright © 2014 NASANYO BLOG