WATU 20 WAUAWA KATIKA SHAMBULIO HABARI KAMILI HII HAPA by nasanyo fortnine

Watu 20 wauawa katika shambulio la guruneti CAR by nasanyo fortnine

Serikali ya Jamhuri ya Afrika ya Kati imetangaza kuwa, watu 20 wameuawa katika shambulio la guruneti lililoulenga mkusanyiko wa watu waliokuwa katika mazishi mjini Bangui, nchini humo. Hayo yamethibitishwa na Wizara ya Usalama wa Jamii nchini humo na kuongeza kuwa, serikali inalaani vikali shambulizi hilo na imetaka kufanyike uchunguzi wa haraka ili kuwabaini wahusika wa jinai hiyo na kuwapandisha kizimbani. Shambulizi hilo limetokea katika hali ambayo Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limeonya kuwa, askari wa kimataifa wa kulinda amani nchini humo, ndio tu wanaoweza kutoa ulinzi kwa Waislamu wanaoendelea kushambuliwa na wanamgambo wa Kikristo wa Anti-Balaka ambao Umoja wa Afrika umewatangaza rasmi kuwa ni magaidi. Volker Turk mmoja wa viongozi wa shirika hilo ambaye ametoka nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati hivi karibuni, amesema kuwa, kiwango cha chuki za kidini kilichopo nchini humo, kinatia wasi wasi mkubwa. Ameongeza kuwa, kuna tishio kubwa la kumalizika Waislamu katika mauaji yanayofanywa na Anti-Balaka na ametaka kuchukuliwe hatua kali za kukabiliana na wimbi hilo la ukatili na mauaji hayo.

0 comments:

Copyright © 2014 NASANYO BLOG