BAADA YA NDEGE KUTOONEKANA KABISA MAREKANI YAAMUA HIVI habari kamili hii hapa by tuntu baby
by tuntu baby


Juhudi zimeelekezwa sasa katika Bahari Hindi
Marekani imetuma vikundi vya
watalaamu katika bahari Hindi kusaidia katika juhudi za kuisaka ndege ya
Malaysia iliyotoweka, baada ya madai kuibuka kuwa huenda ndege hiyo
iliendelea kupaa kwa zaidi ya muda ambao wachunguzi walidhania hapo
awali.
Maafisa ambao hawakutaka kutajwa wanasema kuwa ndege hiyo ilituma data ya Satelite kwa zaidi ya saa tano baada ya kutoweka.
Hata hivyo wachunguzi walisema data hiyo ya Satelite haijaelezwa kwa kina ingawa serikali ya Malaysia imekanusha madai hayo.
Vyombo vya habari vya serikali ya China
vinadokeza kuwa wataalam wanasema huenda ndege hio ilianguka katika ziwa
la kusini mwa Nchi hiyo .
Hata hivyo maafisa wa Marekani wanaosaidia
katika upelelezi huo wanasema kuwa huenda ndege hiyo ilikuwa ikituma
mawasiliano kwa Satelite hata baada ya kutoweka Jumamosi na kwa hivyo
wanaelekeza juhudi zao Magharibi mwa bahari hindi.
Afisa mkuu wa mauzo wa shirika hilo la ndege Hugh Dunleavy amepuuzilia mbali ripoti hizo.
Serikali imesema kuwa msako wa ndege hiyo utaendelea hadi eneo la Magharibi katika bahari Hindi.
Waziri wa usafiri, (Hishammuddin Hussein)
amekataa kuzungumzia ripoti za Marekani kuwa Ndege hiyo iliendelea kupaa
kwa saa kadhaa kabla ya kutoweka.
Mkuu wa Halmashauri ya usafiri wa ndege nchini
Malaysia, (Azharuddin Abdul Rahman) amesema kuwa Malaysia inashirikiana
na Marekani kubaini ikiwa kuna taarifa zozote za Satelite ambazo
zinaweza kusema iliko ndege hiyo iliyotoweka ikiwa imebeba watu 239.
0 comments: